Tuesday 8 May 2012

Kutana na kabati lililotengenezwa kwa Computer


Watu wengi hufikiri kuwa computer ikiharibika inapoteza umuhimu wake. Lakini kundi la vijana kutoka chuo cha Eden Centre kilichopo kijiji cha Nyakasimbi, Tanzania wamegundua matumizi mbadala badala ya kutupa computer mbovu hasa Central Processing Unit (CPU).

Vijana hao wameibalidisha  C.P.U hizo zilizoharibika kuwa kabati ya kuwekea vyombo, vyakula n.k

Issa Ismail mwanafunzi wa chuo hicho anasema “Kabla ya ugunduzi huu tulikuwa tunatumia meza, ambayo ilionekana kutokuwa na usalama kiusafi, tukafikiria kuwa tunaweza kutengeneza kabati za ukutani kwa kutumia CPU mbovu zilizokuwa zimeandaliwa tayari kwenda kutupwa”.


Mwanafunzi huyo Issa (25) wa chuo cha kilimo na mifugo anaongeza kuwa, kwa kuwa CPU hizo zinaweza kubandikwa ukutani hivyo kuweza kutunza vyombo vyao kwa usafi zaidi ya meza waliyokuwa wanatumia  mwanzo.

No comments:

Post a Comment